26/11/2014
Kila mwananchi anao wajibu wa kusimamia
na kutii kikamilifu sheria za nchi.
Usalama barabarani ni jukumu la kila
mmoja wetu, hivyo kutii sheria za barabarani
iwe ni utamaduni kwa wananchi
wote hususan madereva kwa lengo la
kulinda maisha ya watu na mali zao.
Tujijengee utamaduni wa kutii sheria bila
kushurutishwa.
Polisi wana kazi ngumu na muhimu sana
ya kusimamia sheria. Lazima
kushirikiana nao, isipokuwa k**a
wanatenda kinyume na sheria.
Maelezo hayo ni muhtasari wa mwongozo
wa nini ofisa wa polisi aliyevaa sare
anaweza kufanya kisheria na kukueleza ni
wakati gani anakusimamisha uwapo barabarani.
Unaweza ukapenda kukata
maelezo haya na kuyaweka kwenye gari
lako – lakini kumbuka kwamba ni
mwongozo tu.
Mamlaka ya kusimamisha gari lako:
Ofisa wa polisi ana haki ya kusimamamisha
gari lako – k**a atakupa ishara ya
kusimama, punguza mwendo kwa
usalama na utoke barabarani – pia
anaweza kukuuliza jina na anwani yako
na ile ya mmiliki wa gari (Sheria ya
Usalama Barabarani (RTA), s.78).
Leseni ya kuendesha gari: Ofisa wa
polisi anaweza kuomba kuona leseni yako
ya kuendesha gari – anaweza kukataa
fotokopi – hata hivyo, unaweza kuamua
kupeleka leseni yako ndani ya siku tatu
kwenye kituo cha polisi kilichochaguliwa
na ofisa. Ili kuepuka matatizo, wakati wote
tembea na leseni yako kwenye gari (RTA
s.77).
Hati ya usajili: Ofisa wa polisi ana haki
ya kukagua maelezo ya usajili k**a
yanavyoonyeshwa kwenye kibandiko cha
usajili – gari lazima liendane na maelezo
ya kwenye kibandiko, lakini vitu vidogo
k**a rangi iliyofifia au iliyobanduka
haijalishi (RTA s.13).
Leseni ya barabarani, na bima ya gari:
Ofisa wa polisi ana haki ya kukagua k**a
umebandika leseni halali ya barabarani na
kibandiko cha bima kwenye kiwambo cha
upepo cha gari lako (kioo che mbele).Kunyang’anywa: Ofisa wa polisi HANA
haki ya kuondoa vibandiko na kuchukua
leseni isipokuwa kwa mujibu wa sheria.
Matumizi ya taa nyakati za usiku:
Sheria ya usalama barabarani inakutaka
kupunguza mwanga wa taa za gari lako
unapopishana au kutaka kulipita gari la
mbele yako ili kumwezesha dereva
mwenzako kuyaona vizuri mazigira ya
barabara anayotumia (RTA s.39).
Kuendesha baada ya kunywa pombe:
K**a ofisa wa polisi anakuhisi
umekunywa pombe na huwezi kulidhibiti
gari ipasavyo, anaweza kukutaka upimwe
(kipimo cha kupumua au kipimo cha
damu) kuona k**a kiasi cha pombe
kwenye damu yako ni zaidi ya kiwango
kilichoelezwa. K**a ukikataa utakuwa na
hatia ya kosa (RTA s.44, s.45, s.46).
Kutumia simu ya mkononi wakati
unaendesha: ingawa sheria haikatazi hili
mahususi, ofisa wa polisi anaweza kuona
kuwa unatenda kosa la “kuendesha kwa
uzembe” (RTA, s.42, s. 50).
Mwendo kasi: Unapaswa kuzingatia
kikomo cha mwendo kasi, (ikiwa ni
pamoja na km 50 kwa saa katika maeneo
ya hatari, ambayo yanaweza yasiwe na
alama) – ofisa wa polisi anaweza kupima
mwendo kasi wako kwa namna
mbalimbali - hata hivyo, unaweza kupinga
ushahidi wake mahak**ani (RTA s.51,
s.73(2)).
Kustahili kuwepo barabarani: Ofisa wa
polisi ana haki ya kukagua k**a gari lako
liko katika hali ya usalama kiufundi.
Matairi, breki, taa, indiketa na usukani
lazima viwe vinafanya kazi vizuri –
unaweza kutakiwa kupeleka gari mahali
litakapokaguliwa kikamilifu na mkaguzi wa
magari wa polisi (RTA, s.39.1, s.81).
Unashauriwa kupeleka gari lako
kukaguliwa na polisi kila mwaka. Pata
stika ya usalama barabarani, cheti cha
ubora wa gari, au barua kutoka polisi
k**a ushahidi kwamba gari lako
limekaguliwa.
K**A OFISA WA POLISI ANAKUTUHUMU
KWAMBA UMEFANYA KOSA:
Mara nyingi utapewa uchaguzi wa
kukubali kosa na kulipa faini ya sh. 30,000
kwa ofisa wa polisi, au kwenda mahak**an
ili kujibu mashtaka. Ofisa ataandika
maelezo kwenye Fomu ya Polisi ya PF
101, na nyote wawili mtatia saini – kamwe
usilipe faini bila ya kupata nakala ya Fomu
iliyotiwa saini. Unaweza kwenda na ofisa
kwenye kituo cha Polisi kutoa maelezo.
K**a unakubali kosa, lakini huwezi kulipa
faini, ofisa wa polisi atakueleza jinsi ya
kutuma malipo kwa k**anda wake wa
eneo (RTA, s.95).
K**A UNAFIKIRI OFISA WA POLISI
AMETENDA KINYUME CHA SHERIA AU
AMEKOSEA KWA NJIA YOYOTE
UNAWEZA KUTOA MALALAMIKO:
Muulize ofisa jina lake, cheo na namba,
na anwani ya kituo cha polisi anakofanyia
kazi (unayo haki ya kuuliza hilo.) Kisha
peleka malalamiko ya maandishi kwa
Mkuu wa Polisi wa eneo husika au kwa
K**anda wa Kikosi cha Usalama
Barabarani, S. L. P 1712, Dar es salaam –
ambaye atachunguza na kujibu.
Tusaidie kuwafanya maofisa
polisi wetu kuwa waaminifu –
usitoe rushwa na usipokee
rushwa.
Said A. Mwema
Inspekta Jenerali wa Polisi
10/6/2011
Jeshi la Polisi Tanzania na Wizara ya
Ujenzi – wanashirikiana kwa ajili ya
usalama zaidi wa barabara.
UMESIMAMISHWA NA POLISI WAKATI UKIENDESHA?
ZIJUE HAKI NA WAJIBU WAKO!