Maurice Njowoka

Maurice Njowoka Ushauri Kuhusu sheria,haki na wajibu

30/04/2021

UGONI NI NINI
Na wakili Asajile Baraka
✅kujamiiana kwa hiari kati ya mwanamume na mwanamke ambao hawajaoana lakini angalau mmoja wao ni mtu aliyeolewa/kuoa. Kwa tanzania ni kosa la madai. Ni muhimu kuwa na ushahidi kuwa mkeo au mumeo alijamiana na mwanaume au mwanamke mwingine. Sms tuu hazitoshi lakini kuwe na ushahidi kuwa walifanya mapenzi

MAMBO MUHIMU KUDHIBITISHA KWA KOSA LA UGONI/ELEMENTS TO ESTABLISHED.
✅1) kwamba mwanamke ameolewa au mwanaume kaoa;
✅ 2) kwamba anafanya ngono na mwanaume sio mumewe au mwanamke asiye mkewe
✅ 3) kwamba kwa habari ya mwanamume ambaye alifanya tendo la ndoa naye, lazima amjue kuwa ameolewa.
,✅4.) Kupewa mimba na mume wa mtu na kumpa mimba mke mtu
✅5.) Magonjwa ya zinaa
✅6.) Fumanizi la papo kwa papo

UTETEZI WA UGONI/DEFENSES FOR ADULTERY.
✅Kuna utetezi wa aina tatu unaweza kutumika katika kesi za ugoni
1.Fumanizi la ugoni la kupanga,
Hii hasa kwa wale ambao wanapanga na mke wake anatafute buzi then ajifanye anamfumania mke wake.
Huu unaweza kuwa utetezi k**a jamaa akagundua kuwa kumbe mlipanga fumanizi la ugoni dhidi yake.
2.k**a mume au mke tayari mmepeana talaka.
K**a mmeshaachana kwa talaka huwezi msh*taki mwanandoa mwenzako kwa ugoni hata umfumanie.
3.K**a mwanaume alikuwa hajui kuwa anayejamiana naye ni mke wa mtu, au mwanamke alikuwa hajui kuwa aliyekuwa anafanya naye mapenzi ni mume wa mtu huu unaweza kuwa utetezi.

Soma S.72 of LMA RE 2019.

It is not exhaustive, mcheki mwanandishi kwa elimu zaidi au wasiliana na Mwanasheria wako.
Mwandishi hatahusika na matumizi mabaya ya elimu. Hii ni mwongozo
0755845107
0784745645
Zote zipo WhatsApp.

26/04/2021

NAMNA YA KUOMBA UMILIKI ARDHI VIJIJINI

Sehemu ya pili

Maombi ya kumiliki ardhi kupitia katika Ardhi ya Kijiji hupatiwa
Hati Miliki ya Kimila na hufanywa katika ardhi ya kijiji.

Maombi hayo hupelekwa kwa mtendaji wa serikali ya kijiji ambaye yupo
katika eneo la vijiji.

Kwa maana nyingine Hati Miliki ya Kimila
hupatikana katika ardhi ya kijiji.

NA ufuatao ni utaratibu wa
kupata Hati Milki ya Kimila:

i). Maombi yake yatafanywa katika fomu maalum na yatatiwa
saini na mwombaji; au yatatiwa saini na watu wasiopungua wawili kutoka katika familia k**a maombi hayo yatakuwa
yamefanywa na familia;

au watu wasiopungua wawili iwapo maombi yamefanywa na kikundi cha watu.

ii) Maofisa wadhamini wasiopungua wawili k**a maombi ni ya chama chama cha ushirika;

iii). Wanakijiji wasiopungua watano na wasiokuwa ndugu wa yeyote iwapo maombi ni ya kundi la watu wasio wakazi wa kijiji hicho

iv). Wakala aliyeidhinishwa.

BAADA YA MWOMBAJI KUTIMIZA MATAKWA HAYO KATIKA MAOMBI HATUA INAYOFUATA ni;-

i). Mwombaji aambatanishe tamko la ardhi nyingine anayoimiliki nchiniTanzania;

ii). Maombi yaambatanishwe na nyaraka na taarifa nyingine zilioanishwa;

iii). Maombi yaambatanishwe na ada;

iv). Tamko la nia ya kuanzisha ujenzi wa makao katika miezi mitatu iwapo waombaji si wakazi wa kawaida wa kijiji;

v). Maombi yawasilishwe katika serikali ya kijiji au ofisa wake muidhiniwa na ndipo;-

Halmashauri ya kijiji itafanya uamuzi juu ya maombi hayo kabla
ya kupita tangu iyapokee maombi hayo au siku tisini baada ya kupokea taarifa ya ziada.

SOURCE:

Cases;
NAFCO VS MULBADAW VILLAGE COUNCIL AND OTHERS (1995) TLR 88

Sheria zinazotumika;
Section 22 of village land Act
Section 17 of village land Act
Section 19 of village land Act
Section 23 of village land Act
Section 24 of of village land Act
Section 25 of of village land Act

Je mwanamke anaweza kuwa hatiani kwa kosa la mumewe , na je polisi anaruhusiwa kumk**ata na kumshurutisha mke kwa kosa l...
22/04/2021

Je mwanamke anaweza kuwa hatiani kwa kosa la mumewe , na je polisi anaruhusiwa kumk**ata na kumshurutisha mke kwa kosa la mumewe............hivi karibunii ntakupa elimu hii ujikomboe

16/04/2021

Kuna muda mungu uleta moto, ili hali matarajio yetu tuliitaj maji kunamuda tunapitia hali na matukio yaliyotuumiza mno ila kumbe n mungu alkuwa nyuma yetu... yake sio k**a yetu tusijute...bado kidogo tutafikaa..God made us for reason

28/03/2021

UTETEZI WA KUTOKUWEPO WAKATI WA TUKIO LA KIHALIFU LINAPOTENDEKA/DEFENCE OF ALIBI.
Na mwandishi wetu wakili Asajile Baraka
👉Mara nyingi mtuhumiwa amekuwa akijitetea kuwa hakuwepo wakati tukio la uhalifu limetokea. Hivyo yeye hausiki na Hana hatia kwa Sababu wakati Hilo tukio linatendeka yeye hakuwepo.
👉Pale ambapo mtuhumiwa anataka kutumia/ kutegemea utetezi wa alibi kabla ya kusikilizwa kwa kesi hiyo, atatakiwa kutoa upande wa mashtaka na maelezo ya utete huo wakati wowote kabla ya kesi ya upande wa mashtaka kufungwa.
👉 Pia atatakiwa kutoa viambatanisho au vielekezo vivyothibitsha kuwa hakuwepo eneo la tukio wakati uhalifu ulipokuwa ukitendeka.
Atatakiwa kufanya hivyo baada kutuma taarifa kwa Mahak**a kuwa anataka kutumia utetezi huo.

👉K**a hatazingatia matakwa haya k**a inatajwa na Sheria k**a ilivyo elezwa Basi utetezi wake hautakubalika.

👉K**a unataka kutumia utetezi wa namna hii bhasi lazima uijulishe Mahak**a mapema Sana iwezekanavyo kabla kesi ya upande wa mwendesha mash*taki haujafunga kesi/ before prosecution case closed.
You should've done it at earliest stage as possible that you want to defend yourself with a defence of alibi

Hii Ni kwa Mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai kifungu 194(4)(5) (6)

Toa maoni yako. Kwa comment.
Imechapishwa Mwanasheria Online
0755845107
0784745645
Follow me on Instagram.
Usisahau kulike page kwa elimu zaidi.

28/03/2021

MAMBO YA MSINGI NA TARATIBU ZA KUFANYA UPEKUZI(SEARCH WARRANT)
Sehemu ya kwanza.
Wakili Asajile.
1.Kuingia na kufanya upekuzi ndani ya nyumba kutafanyika tu, endapo:
(a)Kuna hati ya Upekuzi iliyotolewa (Search warrant)
(b)Katika kutekeleza nguvu za kisheria zilizotolewa kwa maafisa Fulani wa Polisi kuingia
(c) ndani na kufanya upekuzi bila ya hati ya kupekulia.
✅Hakuna mazingira yoyote ambayo polisi aweza kuingia ndani ya majengo binafsi labda tu ana hati ya kufanya upekuzi au amepewa nguvu maalum zinazopatikana katika sheria mbalimbali za Tanzania kuingia
KUINGIA NA KUFANYA UPEKUZI UKIWA NA HATI
(a) na kufanya upekuzi. Endapo Mkuu wa Kituo cha Polisi, Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya au Afisa wa Upelelezi anadhani ni muhimu kuingia katika majengo binafsi ili kupata mali au kitu chochote ambacho, au kuhusiana n a kosa lililofanyika, au kitu chochote ambacho ni muhimu katika upelelezi wa kosa lolote, ataomba mahak**ani hati ya upekuzi chini ya kifungu cha 38 cha Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, Sura ya 20 mapitio ya mwaka 2019.
✅Mtu aliyetajwa katika hati ndiye atakayefanya upekuzi. K**a upekuzi utafanyika kati ya masaa ya machweo ya jua au mawio, Hakimu ataombwa kuidhinisha kufanyika kwa upekuzi huo saa yoyote ya mchana au usiku (kifungu cha 40 cha Sheria ya mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20. Iwapo Afisa aliyeelezwa hapo juu amepata taarifa na anazo sababu za kuamini kuwa mtu anayetafutwa kuhusiana na kutenda kosa la jinai yupo ndani ya nyumba yoyote, ataomba hati ya kumk**ata kwa Hakimu wa eneo husika.
✅Iwapo kitu chochote kimechukuliwa kutokana na upekuzi uliofanyika, afisa aliyechukua vitu hivyo atatoa risiti kuonyesha kuwa vitu hivyo vimechukuliwa, ikiwa na sahihi ya ya mmiliki wa jengo au ndugu wa karibu au mtu mwingine anayemiliki jengo kwa wakati huo wa upekuzi kma yupo yeyote. na sahihi za mashahadi wakati Maafisa wa Polisi wanakumbushwa kuwa kifungu cha 38 (4) cha Sheria ya Mwenendo wa jinai.

Zingatia kutoka kwa lawyer Njowoka
03/08/2020

Zingatia kutoka kwa lawyer Njowoka

24/06/2020

LEO NATAKA TUJOKUMBUSHE
pale unapok**atwa nakufkishwa kituon kuna kuandika maelezo zingatia
1.Askar anatakiwa akwambie kuwa n hak yako kuleta yule na kuandika kile uonacho n part ya ukwel wako
2.muda ..zingatia hii uchukuliwa ndani ya Massa 4 tu kutoka kitabu CPA kifungu 50,51
3.Muda was kuchukua hii na kumaliza unatakiwa kuandika kifungu cha 57(2)e
4.Uthibitisho kuwa umeridhika na umesoma ni sain ya ww mshtakiwa
5.Askar pia anatakiwa aandike key muhimu ushahid kitabu cha ushahid mstar kifungu 27
6. Baada ya kukiri kwa nia na Uhuru binafs kuwa yupo tayar kupelekwa kukiri mbele ya msimamizi wa haki
**Tambua hii utumika k**a ushahid wa kwanza utarudiwa ila kiri k**a ulichukuliwa kwa nguvu au haukuwa wa haki kitabu cha ushahid sura kifungu 27(1,2)

Je wajua kuchapisha, kutoa taarifa za uongo, kutusi au za kuchochea n kosa kisheria # kutoka kwenye kitabu cha sheria za...
22/06/2020

Je wajua kuchapisha, kutoa taarifa za uongo, kutusi au za kuchochea n kosa kisheria
# kutoka kwenye kitabu cha sheria za mitandao za mwaka 2015 kifungu cha 16

Address

Malimbe
Mwanza

Opening Hours

09:00 - 17:00

Telephone

+255654937157

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maurice Njowoka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Maurice Njowoka:

Share

Category