Hekima Ya Ushujaa

Hekima Ya Ushujaa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Hekima Ya Ushujaa, Legal Service, Kihonda Bima, Morogoro.

Hiki ni kipnd ambacho kitakujia mara kwa mara kinachohusisha utoaji wa mawazo yenye hekima ndani yake ambayo inajumuisha maandiko, ili kuwez kumwakwamua mtu kutoka ngazi moja hadi nyengine kimawazo, k

10/10/2022

SEMA, NIFANYE/NITENDE
Je! Ulishawahi kusikia watu wakisema kuwa "kusema ni dawa?". Jibu ni ndio, mara nyingi huwa tunataman vitu vingi na vikubwa ila huwa hatusemi, tunatumia bidiii na nguvu kubwa ktk kuvitafuta bila kusema eti tu unaamini kuwa hicho kitu ni huenda kikawa kidogo ukakimalisha mwenyewe, lakini matokeo yake huwa sivyo. Kitabu cha Mwanzo 7:7 kiaelezea kabisa juu ya kusema. "Ombeni mtapewa..." kwa lugha rahisi ni kwamba, usiposema hutopewa. Fikiria tu ktk maisha ya kawaida, je mtu anaweza kuja na kukupa hitaji la moyo wako bila ya kumuomba/kusema? Jibu ni hapana. Hivyo hata kwa Mungu yatupasa kusema/kuomba ndipo tupate. Unaposema unatengenez jambo jipya ambalo ulitaka litokee ama liwepo. Ikiwa Mungu Ali ufanye ulimwengu kwa kusema/neno, basi yatupasa na sisi tuseme siku zote wala tusikate tamaa, ili tupate haja za mioyo yetu. Mungu Akubariki sana.

07/10/2022

BADILI SHERIA YA MAISHA YAKO
Sheria k**a sheria huwa ni kanuni au mtiririko wa kufuata ktk jambo fulani, na pindi inapoekwa huwa si rahisi kubadilika, huwa inafuatwa. Na ndio maana ukawa unaskia watu wakisema sheria ni msumeno, kwa maana ya kwamba pindi imewekwa hakuna bud kuifuata.
Hivyo ktk maisha ya kila mwanadamu kuna sheria ambazo zimewekwa, maneno ya watu ni k**a sheria kwenye maisha yako. Ikiwa unataka kufikia hitaji lako, lazima ubadilishe sheria usiyoihitaji ambayo imewekwa kwenye maisha yako.
Kuna watu walijihatarisha na kusema "liwalo na liwe" au "potelea pote" kwa kuamua kweli kweli.
Usipojihatarisha kuamua, sheria itakufunga kwenye maisha yako.
BE A LAW CHANGER.

07/10/2022

UONGOZI HALISI NI UTUMUSHI
Utumishi ni ile hali ya mtu kukubali kutumika kwa namna moja au nyengine. Ktk uongozi wengi wamekua na dhana kuwa pindi uwapo mkuu (kiongozi) huwa ni wa kutuma tu na sio kutumika.
Yesu mwenyewe katika kitabu cha Luka 22:27
Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni k**a atumikaye. Kristo ambae mkuu anathibitisha kuwa uongozi (ukuu) ni kutumika, ikiwa yeye aliye mkuu alitumwa na akakubali kutumika, hivyo inatupasa kutumika pindi tuwapo wakuu.
Lakini pia kiongozi huwa anapaswa aonyeshe mfano hasa kwa matendo ili kuweza kutimiza utumishi uliotukuka. Ktk kitabu kile cha Yoh 13:12-17. Yesu mwenyewe alionyesha mfano kwa wanafunzi wake kwa kuwatawadha miguu haliyakiwa alikuwa ni mwalimu, Bwana n.k. Ndipo Alipowaambia "Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.
Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili k**a mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo." Hivyo sifa kuu ya uongozi wa utumishi ni kuongoza kwa mfano.
Kunahitaji moyo juu ya uongozi wa utumishi kwa kuwa una-:
1. Unahitaji kuhamasisha na kushawishi
2. Unatumia nguvu binafsi
3. Watu wanafanya kitu kwa sababu wanataka
4. Kunawekeza zaidi muda na nguvu.
5. Watu hufanya jambo zaid ya matarajio n.k
Hivyo, ni maombi yangu, dua zangu na sala zangu pindi uwapo kwenye wito wa uongozi huu pendelea kujinyenyekeza na kuonyesha mifano ktk kuingoza kwako, Mungu Atakufanikisha. Mithali 15:33.

23/09/2022

NGUVU YA MASHAURI.
Katika maisha ya siku za leo, watu wengi tunatafuta hekima kwa namna moja ama nyengine, lakini tatizo kuu ambalo wengi hawajui ni kwamba moja ya vyanzo vikuu vya hekima ni pamoja na kukubali mashauri au ushauri ambao watu wanatoa kwa moyo na kwa mafanikio kitabu cha methali kinasema kwenye sura ya 12:15
[15]The way of a fool is right in his own eyes: but he that hearkeneth unto counsel is wise.
Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
Hii inamanisha kuwa katika kupata hekima ni lazima ujinyenyekeze kwenye kukubali na kupokea mashauri maana ndio yanayotujenga na kutuongezea mbinu mpya za suluhu, au utatuzi wa mambo au hata njia mbadala ya mafanikio.
Kuna msemo unasema kupotea njia ndio kujua njia, hii inamana kwamba ktk kukosea kunaleta ujuzi, hivyo ktk ujuzi unaopewa na mtu aliekosea upokee na uutilie maanan kwa ajili ya kufanikisha hitaji lako.
Naomba uwe ni mtu mwenye kukubali mashauri ( be submissive) ili kuwa na hekima ya kufanya mambo.
-Frank Manda-

14/09/2022

HERI LAWAMA
Watu wengi siku za leo wamekua wakichukia kitendo cha lawama, mafundisho ama kwa namna nyengine tunaina marekebisho ama maonyo, bila kujua kuwa njia pekee ya kuimarika ktk kufanya japo kwa ufanisi ama ufasaha ni mafundishi, marekebisho ama maonyo.
Lawama, Mafundisho, marekebisho ama maonyo yanafaida nyingi sana ktk maisha ya kila siku, maandiko matakatifu yanatuambia ktk kitabu cha Mithali 12:1" Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa, bali yeye achukie kulaumiwa ni k**a mnyama" hivyo moja ya umuhimu wa Mafundisho, marekebisho ama maonyo yanaleta maarifa ktk maisha, na kazi ya maarifa husaidia kumfanya mtu kuwa na uelewa wa kufanya jambo kwa umakini, kwa kujua hata athari inayowez kujitokeza ktk kitu afanyacho na kuweza kuishuhulikia.
Hivyo, ni ombi langu kwako ww unaesoma, Penda mafundisho, Marekebisho na hata maonyo. Wakati mwengine kubali pia lawama, kwani katika lawamai utapata Faida ya kuweza kutambua kosa ulilolifanya. Huenda ulilaumiwa katika kuingilia jambo ambalo hukupaswa kuingilia matokeo yake ukalaumiwa.
Hapo utapata kujifunza kuwa sio kila kitu unapaswa kukabiliana nacho, hivyo ni matumaini yangu kwamba utakubali lawama, maonyo ama marekebisho ili kuweza kutambua kosa na kulirekebisha likawa na faida kubwa ya kuweza kukuvusha kutoka ngazi moja hadi nyengine.
Mungu Akubariki. Manda

Send a message to learn more

Address

Kihonda Bima
Morogoro

Telephone

+255629867163

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hekima Ya Ushujaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hekima Ya Ushujaa:

Share

Category