21/12/2023
NIA NJEMA KWA NJIA MBAYA.
Huu ni mgogoro wa vizazi vingi. Wana maadili na Wana falsafa wamehangaika nao bila makubaliano. Na sidhani k**a suluhu yake inahitajika. Mvutano kati ya Nia njema katika njia mbaya unatusaidia kujifunza kuishi na tusiowapenda.
1. Ukikaza maridhiano punguza ukali wa sheria. Huwezi kupata vyote. Sheria ni msumemo, sharti ikate kote na haina macho.
2. Ukikaza sheria, achana na maridhiano, panua magereza. Wafungwa wakiwa wengi kuliko walio huru, wafungwa wanakuwa huru kuliko Askari magereza.
3. Demokrasia ni muktadha (context), matunda yake (values) ni ya mahali pote (universal). Tubishane juu ya umbo la demokrasia, tukubaliane juu ya matunda.
4. Mafanikio ya utendaji wa hospitali si ongezeko la wagonjwa. Demokrasia si wingi wa vyama vigonjwa. Hata kimoja kizima kinatosha. Uzima wa mbwa tuupime bila mnyororo. Kwa mnyororo hata mbwa wa mfalme ni mgonjwa.
5. Kutosamehe ni sawa na kunywa sumu ukitegemea afe mbaya wako. Kusamehe ni kujitangazia uhuru kuliko kumtangazia uhuru unayemsamehe. Wanaoomba msamaha, wasamehewe. Wanaoomba kufutiwa mashtaka wafutiwe. Kwenye mvutano, anayekubali kushindwa ndiye MSHINDI.
MAMA ANA NIA NJEMA; TUMTUE GUNIA LA MISUMARI. ALIYEBAKI KITANDANI NDIYE HUTANDIKA KITANDA.