LEGAL AID Clinic

LEGAL AID Clinic Legal Aid Clinic is a community based organization that deals with provision of Legal services free of charge to the people with lower income

MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMAMahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wa...
04/04/2022

MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMA

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wafanyakazi (Commission for Mediation and Arbitration-CMA) haina mamlaka ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi zinazohusu migogoro ya wafanyakazi wa umma.

Kupitia kesi ya rufaa ya madai CIVIL APPEAL NO. 12 OF 2022
TANZANIA POSTS CORPORATION VERSUS
DOMINIC A. KALANGI mahakama hiyo ya juu zaidi ya Tanzania imesema migogoro ya wafanyakazi wa umma inatakiwa kuishia ndani ya Serikali, pale mfanyakazi anapofukuzwa kazi na mkuu wa idara au shirika la Serikali anatakiwa kukata Rufaa kwenda Tume ya Utumishi wa Umma, na endapo mfanyakazi atakuwa hajaridhika na maamuzi ya Tume ya Utumishi wa Umma basi anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa
Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)

Dominic A. Kalangi alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Posta ( Tanzania Posts
Corporation), mwaka 2017 ajira yake ilisitishwa Kwa utovu wa nidhamu. Dominic alipeleka malalamiko yake CMA na kushinda kesi. Shirika la Posta lilikata Rufaa Mahakama kuu Mtwara ambapo pia Dominic alishinda kesi na mahaka kuu ikaamuru Shirika la Posta limlipe fidia Kwa kusitisha mkataba wake wa ajira pasi na kufuata utaratibu.

Kwa Mujibu wa sheria Shirika la Posta la Tanzania ni Mali ya umma linalomilikiwa na serikali hivyo wafanyakazi wake ni watumishi wa umma.

29/09/2021

We are back on air now

Sasa tumerudi hewani

Let's Talk
26/07/2021

Let's Talk

Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi
19/09/2020

Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi

COMPANY LIMITED BY GUARANTEE CAN NO LONGER OPERATE AS NGOs( All Companies obtained certificate of compliance to be struc...
21/06/2019

COMPANY LIMITED BY GUARANTEE CAN NO LONGER OPERATE AS NGOs( All Companies obtained certificate of compliance to be struck off Register, Registrar has power to strike off companies not complying with the law, Certificate of registration of NGOs valid for 10 years only subject to renewal)

Since 31st October 2018 when the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children issued a public statement calling among other things the Non Governmental Organizations(NGOs) registered by other authoritues such as BRELA, RITA to apply for a certificate of compliance to the registrar of NGOs there have been contravesial opinions from various stake holders.

Among the prevailing issues were the following
(a) What would be the status of first registration prior to obtaining certificate of compliance?

(b) The definition of an NGO was narrow

(c) The Definition of a company was narrow

THE PROPOSED AMENDMENT

The Government has come with the bill (The Written Laws (Miscellaneous Amendment ) Act No.3/2019) aiming at amending various provisions of the Companies Act, NGOs Act, Trustees Incorporation Act, the Societies Act and other relevant laws to address the aforesaid legal challenges.

DEFINITION
Section 2 of Companies Act has been amended and the definition of Company has been well elaborated to mean the company formed under the Companies Act for the purpose of investment, trade and commercial activities.

From the wording of that definition it means that a company limited by guarantee carrying out NGOs activities is no longer a company within the meaning of Companies Act.

Furthermore the NGOs Act has been amended by section 2 by strictly excluding all entities registered under other laws such as companies(company limited by guarantee), trust, societies, trade unions, political parties e.t.c

COMPANIES THAT OBTAINED CERTIFICATE OF COMPLIANCE TO BE STRUCK OFF THE REGISTER:

The proposed amendments provide that, all companies, cmpanies limited by guarantee which have obtained the certificate of compliance under section 11 of NGOs Act, shall be struck off the Register of Companies after two months since the coming into force of the proposed law.

POWER TO STRIKE OFF A COMPANY

The proposed amendments have empowered the Registrar of Companies under section 400A of the Companies Act, to strike off any company conducting business contrary to the law. We are of the opinion that through this section most of the companies limited by guarantee conducting NGOs activities without obtaining a Certificate of Compliance under NGOs Act, may be contravening the Companies Act and NGOs Act hence liable to be struck off from the Register of Registrar of Companies.

REGISTRAR OF NGOs AND LAW ENFORCEMENT

The Registrar of NGOs has been empowered to inspect and asses any entity operating as an NGOs. The Registrar has been afforded escort by law enforcement agencies in discharging his duties.

RENEWAL OF CERTIFICATE

The proposed amendments of the NGOs Act direct that the certificate of registration under the Act shall be valid for 10 years subject to renewal. The application for renewal shall be made six months before expiry of the same.

Victory Attorneys International NGOs and Good Governance Unit handles all matters relating to NGOs.

19/06/2019

Tunashauriwa kuandika wosia angali ya uhai wako ili kuepusha matatizo na migogoro katika familia.

HAKI NA WAJIBU WA WANANDOA KATIKA NDOA YA KISHERIA.Leo nimeona vyema Kama itatupendeza kutazama haki, wajibu na stahiki ...
16/06/2019

HAKI NA WAJIBU WA WANANDOA KATIKA NDOA YA KISHERIA.

Leo nimeona vyema Kama itatupendeza kutazama haki, wajibu na stahiki za wanandoa, ambao ndoa zao hutambuliwa kwa mujibu wa sheria yetu ya Tanzania.

Kama ilivyo ada ndoa ni jambo muhimu sana katika jamii zetu, hivyo itapendeza kuwa Kama kila mwanandoa atazitambua na kuzijua haki zake sambamba na wajibu wake.

📎Maana ya ndoa
Ndoa maana yake ni muungano wa hiari kati ya mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu kwa muda wa maisha yao yote (Kifungu cha 9 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971). Ili ndoa hiyo iwe halali hapa nchini inapaswa kufuata matwaka ya Sheria za Tanzania kama:

Muungano lazima uwe wa hiari, muungano uwe ni kati ya mwanamke na mwanaume, muungano huo uwe unakusudiwa kuwa wa kudumu, wafunga ndoa wawe wametimiza umri unaokubalika kisheria, wafunga ndoa wasiwe maharimu (wasiwe watu wenye mahusiano ya karibu ya damu au kindugu), kusiwe na kipingamizi na mfungishaji ndoa awe na mamlaka ya kufungisha ndoa.

Aina za ndoa
Kulingana na Sheria ya Ndoa kuna aina kuu mbili za ndoa; ndoa ya mke mmoja na ndoa ya zaidi ya mke mmoja. (Ifahamike kwa Sheria ya Tanzania mke anapaswa kuwa na mme mmoja tu).

(a)Ndoa ya mke mmoja
Huu ni muungano unaoruhusu mwanamme kuoa si zaidi ya mke mmoja. Mfano, ndoa ya Kikristo.

(b) Ndoa ya zaidi ya mke mmoja
Huu ni muungano unaoruhusu mwanamume kuoa mke zaidi ya mmoja. Mfano, ndoa za Kiislamu na ndoa za kimila.

Sheria ya Ndoa inatambua aina tatu za ufungaji ndoa yaani kiserikali, kidini na kimila. Pamoja na aina za ndoa zilizotajwa hapo juu sheria ya ndoa inatambua dhana ya kuchukulia ndoa hii ni kwamba iwapo itathibitishwa kwamba mwanamume na mwanamke wameishi pamoja kwa muda wa miaka miwili au zaidi na kupata heshima ya mume na mke basi itakuwepo dhana inayokanushika kwamba watu hao walioana ipasavyo. Madhumuni ya dhana hii ni kumwezesha mwanamke na watoto kupata masurufu pale ambapo ndoa inavunjwa.

HAKI NA WAJIBU WA MUME AU MKE KATIKA NDOA.

Baada ya kufunga ndoa na ikaonekana haina kasoro yoyote, mke na mume ana haki mbalimbali kisheria anazostahili kuzipata kisheria. Haki hizi ni kama;

Matunzo
Mke au wake wana haki ya kutunzwa na mume wao kwa kuwapatia mahitaji muhimu kama chakula, malazi, mavazi, matibabu, n.k kulingana na uwezo alionao mume. Hivyo katika ndoa mume anao wajibu wa kumkimu mkewe kwa kumpatia malazi, Nguo na chakula. Mke mwenye kipato vile vile anao wajibu wa kumkimu mumewe ikiwa tu mume huyo:
· Hajimudu kabisa.
· Hawezi kupata chumo la Maisha yake kwa sababu ya athari ya akili au afya mbaya
(hii ni kwa mujibu wa Sheria ya ndoaSura ya 29 ya sheria kifungu 63).

Hivyo basi kisheria mume ndio mwenye wajibu wa kwanza wa kumtunza mkewe. Mke anaweza kumtunza/kumkimu mume ikiwa mume hajimudu i.e hawezi kufanya kazi au shughuli kwa sababu mbalimbali kutokana na athari ya akili au akiwa na afya mbaya. Ikumbukwe mke anaweza kudai kwenye vyombo vya kisheria ikiwemo mahakama kama mume hatampa matunzo.

kutunza watoto
Mume na mke wana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mtoto wao na kumpatia mahitaji muhimu kama chakula, nguo, malazi, elimu na mahitaji muhimu. Ni kosa kisheria kutokumuhudumia mtoto wakati ukiwa na uwezo wa kumhudumia. Makosa hayo ni:

Kutelekeza Watoto
Kwamba mtu yeyote ambaye, ni mzazi au mlezi au mtu mwingine mwenye uangalizi au utunzaji halali wa mtoto yeyote mwenye umri usiozidi miaka kumi na nane, hali ana uwezo, wa kumuhudumia mtoto, kwa kuamua au kinyume cha sheria, au bila ya sababu za msingi atakataa kumhudumia, na akamtelekeza mtoto bila msaada, atakuwa ametenda kosa. Kifungu cha 166 cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya sheria za Tanzania pamoja na kifungu cha 188 cha Sheria ya Mtoto ya 2009.

Kosa la Kupuuza kumpa chakula mtoto n.k
Mtu yeyote ambaye, ni mzazi au mlezi au mtu mwingine mwenye uangalizi au utunzaji halali wa mtoto yeyote mwenye umri usiozidi miaka kumi na nne na asiyejiweza, akakataa au kupuuza (hali ya kuwa anaweza kufanya) kumpa chakula cha kutosha, nguo, malazi na mahitaji mengine ya lazima kwa maisha ya mtoto kiasi cha kumdhuru kiafya mtoto huyo, atakuwa ametenda kosa. Kifungu cha 167 cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya sheria za Tanzania pamoja na kifungu cha 189 cha Sheria ya Mtoto ya 2009.

Umiliki wa pamoja wa mali na mahusiano baina ya wanandoa
Mali ya mke au mume iliyopatikana kutokana na jasho lao wote wawili ni mali yao kwa pamoja hata kama juhudi zao au jasho.

HAKI ZA MWANAMKE KATIKA NDOA

1. Usawa
Sheria ya ndoa katika kifungu cha 56 inatamka bayana kwambamwanamke aliyeolewa ana haki sawa katika kupata, kumiliki na
kutumia mali yake kama ilivyo kwa mwanaume.

Kwa ndoa za wakewengi, wanawake katika ndoa hizo wana haki sawa,

Pia kifungucha 66 kinakataza mwanandoa yeyote kumpiga mwenziwe kwasababu yoyote ile.

2. Matunzo
Kifungu cha 63 kinatamka kwamba mume ana wajibu wakumtunza mkewe kwa kumpa mahitaji yote muhimu katikamaisha kama mavazi, chakula na malazi kulingana na uwezo wake.

Mke pia atakuwa na wajibu huo ikiwa tu mume kwa sababu yaugonjwa hawezi tena kufanya kazi yoyote.

Na kama mumehatekelezi wajibu huo kwa makusudi mahakama chini ya kifungu
cha 115 yaweza kumwamuru kutekeleza wajibu huo.

3. Kumiliki Mali
Mke ana haki ya kumiliki mali aliyoipata kabla ya ndoa.

Ndoahaiwezi kuwa kigezo cha lazima cha kubadilisha umiliki wa mali yamwanandoa isipokuwa tu kama wenyewe wamekubaliana hivyo napia haimzuii mwanandoa kujipatia na kumiliki mali yake binafsiakiwa katika ndoa. Kifungu cha 58 kinaeleza haki hiyo.

4. Kuishi katika nyumba ya ndoa
Mke ana haki ya kuishi katika nyumba ya ndoa. Kifungu cha 59kinaeleza kwamba nyumba ya ndoa ni ile ambayo wanandoawanaishi.

Hii inaweza kuwa nyumba waliyojenga au ya kupanga, Na kama nyumba ya ndoa ni ya kujengwa na wanandoa wenyewe,
basi hakuna mwenye mamlaka ya kuiuza, kuipangisha au kuiwekarehani bila idhini ya mwanandoa mwenzake.

5. Kukopa
Mke ana haki ya kukopa kwa jina la mume wake au kuuza vitu vyamume kwa lengo la kujipatia mahitaji ya lazima ya familia.

6. Uhuru wa kuishi popote
Endapo mume atafariki kifungu cha 68 kinampa mjane haki yakuamua akaishi wapi na asiolewe au aolewe na mtu ampendaye bila
kuingiliwa na mtu au kufungwa na mila yoyote.

7. Kupata haki ya jasho lake
Mke ana haki ya kupata haki ya jasho lake alilochangia kwenyemali iliyopatikana wakati wa ndoa iwapo ndoa itavunjika kama
inavyoelezwa katika kifungu cha 114.

Address

Viwandani Street
Dodoma
333000

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 18:00
Sunday 09:00 - 18:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when LEGAL AID Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to LEGAL AID Clinic:

Share

Category

ACCESS TO JUSTICE IS A RIGHT

“The only true forms of equality are equality at the last judgment and equality before a just court of law; all other attempts at leveling must lead at best to social stagnation” - Russel Kirk