29/09/2022
Talaka ni haki aliyonayo kila mwanandoa. K**a ilivyo haki ya kufunga ndoa ndivyo ilivyo haki ya talaka pia. Yeyote kati ya wenye ndoa anaweza kuomba talaka. Awe mwanamke au mwanaume. Lakini hii ni katika sura ya 29 ya Sheria ya ndoa na si katika imani ya dini yoyote.
1.TALAKA NININI.
Talaka ni amri /tamko maalum la mahak**a linalotamka kuhusu kuvunjika kwa ndoa. Hii ndio maana ya talaka lakini kwa mujibu wa sheria.
Katika maana hiyo twapata kujua kuwa talaka ni lazima itolewe na mahak**a.
Mahak**a ndicho chombo chenye dhamana kuu katika kubatilisha ndoa kwa namna ya talaka.
2. JE UNAWEZA KUOMBA TALAKA MUDA GANI BAADA YA KUFUNGA NDOA.
Ili uweze kuomba talaka ni lazima ndoa itimize miaka iwili . Huwezi kufunga ndoa mwezi huu halafu mwezi ujao ukakimbilia mahak**ani ukitaka talaka. Ndoa ikifikisha miaka miwili basi haki ya talaka inafunguka.
3. TOFAUTI YA KUTENGANA NA TALAKA.
Sio kila kuachana ni talaka. Aina nyingine za kuachana zina sifa za kutengana na sio talaka. Kutengana ni hatua ambapo wanandoa wanaacha kuishi chini ya paa au dari moja. Wanaweza kuishi nyumba moja lakini vyumba tofauti.Halikadhalika wanaweza kuishi nyumba tofauti na hata pakawa mbali ya nchi kwa nchi, mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya,kijiji kwa kijiji n.k.
Tofauti kubwa kati ya talaka na kutengana ni kuwa katika talaka kunakuwa na tamko maalum kutoka mamlaka maalum linalositisha mahusiano ya ndoa, wakati katika kutengana hakuna tamko lolote kutoka katika mamlaka linalotangaza kuisha au kusitishwa kwa mahusiano ya ndoa.
Kutengana kupo kwa aina mbili. Kwanza ni kutengana kwa hiari ambapo wanandoa kwa hiari yao wanatengana, na pili ni kutengana kwa kuiomba mahak**a kuwatenganisha. Yapo mazingira ambapo kumtenga mwenza kunaweza kuwa kugumu kutokana na mazingira kadha wa kadha na hapo ndipo unapoweza kuiomba mahak**a iwatenganishe.
4. UNAPOHITAJI TALAKA FUATA HATUA HIZI.
( a ) Hatua ya kwanza kabisa kabla ya kwenda mahak**ani lazima upeleke ombi lako baraza la usuluhishi wa migogoro ya ndoa. Kwa waislamu baraza hilo ni BAKWATA na wengine baraza hilo ni ustawi wa jamii . Kila makao makuu ya wilaya ustawi huu upo ukiuliza utaelekezwa.
Baraza hili litajaribu kusuluhisha na likishindwa litakuandalia fomu maalum kuhusu kushindwa kwake kusuluhisha. Fomu hiyo inaitwa fomu namba 3.
( b ) Hatua ya pili utakapokuwa umepewa fomu hiyo utatakiwa kuandaa maombi ya kisheria ya kutaka kuvunja ndoa huku ukiambatanisha hati hiyo.
Katika maombi hayo utatakiwa kuthibitisha uwepo wa ndoa halali, sababu inayokupelekea kuomba talaka, watoto mlionao k**a wapo, na mali mlizonazo k**a zipo. Mahak**a itasikiliza na itatoa uamuzi.
5. JE NIENDE MAHAKAMA IPI KUDAI TALAKA.
Shauri la talaka ni shauri la ndoa. Na mahak**a zenye mamlaka ya kusikiliza mashauri ya ndoa ni Mahak**a ya mwanzo, ya wilaya, ya hakimu mkazi na mahak**a kuu. Unaweza kufungua shauri lako katika mahak**a yoyote kati ya hizi. Isipokuwa ni lazima iwe mahak**a ile iliyo katika wilaya yako na mahak**a kuu iwe katika kanda yako.
Imeandaliwa na:
Amiri Addy
0744558776
[email protected]
Tunatoa msaada/ushauri wa sheria bure kabisa.