11/01/2016
Habari za jioni ndugu zangu,
K**a ambavyo tuliahidi kuwa tutakuwa tunatoa tafsiri ya sheria inayoshughulikia shughuli na makosa yanayofanyika mtandaoni, The Electronic Transactions Act, 2015.
ANGALIZO: Tafsiri itakayokuwa inatolewa hapa si ile ya kutoka lugha ya kiingereza kwenda katika lugha ya kiswahili, la hasha. Bali tutakuwa tunatoa maelezo ya jumla ili kila mtu aielewe sheria hii kwa urahisi zaidi.
Katika kutoa tafsiri hii, hatutojihusisha na kutafsiri kifungu cha 1,2 na 3 ambavyo kimsingi ni k**a vifungu vya utangulizi tu. Kutokana na hilo, tutaanza na kifungu cha nne ambacho husomeka k**a ifuatavyo:-
Section 4: RECOGNITION OF DATA MESSAGE. 'A data message shall not be denied legal effect, validity or enforceability on the ground that it is in electronic format'.
Hii ina maanisha kuwa taarifa zote zilizotumwa, zilizohifadhiwa au hata kusambazwa kwa njia za ki elekroniki k**a vile ujumbe mfupi wa maandishi, instagram, WhatsApp n.k zinatambulika kisheria na zinaweza tumika hata katika utoaji wa ushahidi katika kesi endapo tu kile kinachobishaniwa mahak**ani au lile kosa linash*takiwa mahak**ani limetendeka katika moja ya njia tajwa hapo juu au njia nyingine yoyote inayofanana na hizo.
Na msisitizo ni kwamba ushahidi wa aina hii hauwezi kupingwa eti kwa sababu tu uko katika mfumo wa ki elekitroniki.
Imekuwa kawaida sana siku hizi watu kutukanana kwa njia ya simu, au hata mitandao ya kijamii, watu wanaingia makubaliano mbalimbali kupitia simu za mkononi au hata kupitia mitandao ya kijamii. Utapeli mwingi hufanywa kupitia mitandao ya kijamii lakini watu tumekuwa hatujui nini cha kufanya kwa kuamini kuwa hatuna ushahidi wa kile kilichotendeka. Na hii yote inatokea kwa sababu tu tunadharau ujumbe unaotumika katika kufanya utapeli, n.k
Naomba nitoe mfano. Yuko mtu (jina.kapuni) alikuja ofisini kwangu akilalamika kuwa katapeliwa. Kwa mujibu wa maelezo yake, alimkopesha mtu hela kiasi cha Tshs. 45,000,000/=. Lakini mazungumzo yote juu ya kukopeshana kwao yalifanyika kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kutumia simu ya mkononi. Katika kutoa maelezo yake mwishoni ak**alizia kwa kulalamika kuwa hana jinsi kwa sababu hana ushahidi wa
maandishi wa kumbana yule alomtapeli.
Hii inamaanisha kuwa hakujua kuwa hata ule ujumbe walokuwa wanachati ungetosha kabisa kutumika k**a ushahidi katika madai yake dhidi ya yule mtu.
Kwahiyo ndugu zangu, tusijidanganye na wala tusidharau michakato mbalimbali inayofanyika mitandaoni au katika njia za kawaida za simu.
Ukitukanwa kwa njia yoyote ya kimtandao, ukikopwa hela kwa njia ya mtandao au sms za kawaida, ukiingia makubaliano yoyote kwa njia ya mtandao, au kitu chochote unachohisi kinaweza leta mgogoro, hakikisha hufuti huo ujumbe iwe ni katika sms, facebook, instagram, twiter n.k kwani itakusaidia sana.
ANGALIZO. Ili uweze kutumia ujumbe wako kisheria, ni lazima iwe imekidhi vigezo kadhaa ambavyo tutavielezea taratibu katika utaratibu wetu huu.
Kwa yeyote mwenye swali, maoni au hata hoja ya kuongeza ili kufanya hiki kifungu kieleweke vizuri anakaribishwa kuchangia.
Ahsanteni