14/05/2026
WANAFUNZI WA K**E CBE WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI SAHIHI NA UHIFADHI TAULO ZA K**E
Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kupitia Kurugenzi ya Huduma za Wanafunzi kimeendelea kuwawezesha wanafunzi wa k**e kwa kutoa mafunzo kuhusu matumizi sahihi na uhifadhi sahihi wa taulo za k**e zilizotumika.
Mafunzo hayo yaliendeshwa na Bi. Sapiencia Masaga, Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu wa CBE, pamoja na Bi. Irene Felix Masawe kutoka ORA Sanitary Pads.
Katika mafunzo hayo, wanafunzi walipata elimu kuhusu:
✅ Matumizi sahihi ya taulo za k**e
✅ Aina mbalimbali za taulo za k**e
✅ Umuhimu wa usafi binafsi wakati wa hedhi
✅ Namna salama ya kuhifadhi taulo zilizotumika
✅ Madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukosefu wa usafi wakati wa hedhi
✅ Utunzaji wa afya na mazingira wakati wa hedhi
✅ Mafunzo ya vitendo kuhusu matumizi sahihi ya taulo za k**e
Aidha, washiriki walipata nafasi ya kuuliza maswali, kushirikiana uzoefu wao, pamoja na kupatiwa taulo za k**e kutoka ORA Sanitary Pads.
CBE inaendelea kuweka mazingira bora ya kujifunzia kwa kuzingatia afya, ustawi, na maendeleo ya wanafunzi.