Law Reform Commission of Tanzania

Law Reform Commission of Tanzania The Law Reform Commission of Tanzania is an independent institution which was established under the

Law Reform Commission of Tanzania is delighted, and indeed honoured to welcome you all to its Facebook Account. In this account you will be able to find out all that you may wish to know about the Commission. Law Reform Commission of Tanzania traces its inspirational background to the landmark Judicial System Review Commission now nostalgically referred to as the Msekwa Commission. In its report f

iled in 1977, the Msekwa Commission underscored the need for on the need to keep the laws of Tanzania constantly attuned to the changing Tanzanian society. No law, Msekwa Commission pointed out, which is not constantly nourished with new ideas, can be an effective instrument for revolutionary change in any society. Such a law will sooner than later become a mere irrelevance to society.Law Reform Commission of Tanzania Act number 11 of 1980 concretised recommendations of Msekwa Commission and established Law Reform Commission as a law reform agency with wide ranging responsibilities that include to:
1.reform laws of Tanzania so as to bring them to fit changing socio-economic circumstances and aspirations of people of Tanzania;
2.undertake studies and propose reform of the philosophy underlying the various laws;
3.recommend new laws, statutory institutions that give new dimensions to the existing law, and
4.propose new laws, new principles, new remedies, new machinery and to meet the challenges of law as Tanzanian society strive to meet the expectations of every citizen. The Commission was established under the Law Reform Commission of Tanzania Act number 11 of 1980

Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Hafsa Mkwawa Mtasiwa akipokea ‘’Tire Cover ‘’ kutoka kwa Afisa Sheria wa Tume ya Kurekebis...
21/08/2013

Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Hafsa Mkwawa Mtasiwa akipokea ‘’Tire Cover ‘’ kutoka kwa Afisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Mkuu wa Wilaya ya Pangani mkoani Tanga Bi. Hafsa Mkwawa Mtasiwa akizungumza na maofisa wa tume ya Kurekebisha Sheria Tan...
21/08/2013

Mkuu wa Wilaya ya Pangani mkoani Tanga Bi. Hafsa Mkwawa Mtasiwa akizungumza na maofisa wa tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ofisini kwake.

Katibu Twala wa Mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan akipokea ‘’Tire Copver’’ kutoka kwa Afisa Sheria wa Tume ya Kurekeb...
21/08/2013

Katibu Twala wa Mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan akipokea ‘’Tire Copver’’ kutoka kwa Afisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha SheriaTanzania Bw. Fredy Kandonga

KatibuTawala wa mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan (Kushoto) akizungumza na maofisa wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanz...
21/08/2013

KatibuTawala wa mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan (Kushoto) akizungumza na maofisa wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ofisini kwake.

06/08/2013

Tume ya Kurekebisha Sheria yashiriki wa Maonyesho ya Nanenane kwenye viwanja vya Nzuguni, Dodoma kuanzia tarehe 01-08/08/2013. Tembelea banda letu lililo karibu na Banda la Tigo hapa viwanja vya Nzuguni, Dodoma. Pata taarifa kuhusu taarifa za maboresho ya sheria Tanzania.

Mwenyekiti wa Tume Jaji Aloysius Mujulizi akimkabidhi ripoti Mapition ya Mfumo wa Sheria unaosimamia Haki za Madai na Ta...
12/07/2013

Mwenyekiti wa Tume Jaji Aloysius Mujulizi akimkabidhi ripoti Mapition ya Mfumo wa Sheria unaosimamia Haki za Madai na Taarifa juu ya sharia za Mila kwa Makabila yanayofuata Mkondo wa Mama Waziri wa Katiba na Sheria Mh Mathias Chikawe

Waziri wa Katiba na Sheria Mh Mathias Chikawe akiangalia moja ya ripoti alizokabidhiwa na Tume wakati Tume ilipokabidhi ...
12/07/2013

Waziri wa Katiba na Sheria Mh Mathias Chikawe akiangalia moja ya ripoti alizokabidhiwa na Tume wakati Tume ilipokabidhi ripoti mbili za Mapitio ya Mfumo wa Sheria unaosimamia Haki za Madai na Sheria za Mila kwa Makabila yanayofuata Mkondo wa Mama

12/07/2013

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DK JAKAYA MRISHO KIKWETE AMUAPISHA JAJI ALOYSIUS MUJULIZI KUWA MWENYEKITI WA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemuapisha Mh. Jaji Aloysius Mujulizi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania. Hafla fupi ya kuapishwa Mh. Mujulizi ilifanyika Ikulu Dar es Salaama na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Mohamed Gharib Bilali, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Benard Membe na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju.
Mh. Jaji Mujulizi anachukua nafasi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mh. Jaji Profesa Ibrahim Juma ambaye sasa ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahak**a ya Rufaa Tanzania.

12/07/2013

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YAKABIDHI TAARIFA ZAKE MBILI KWA WAZIRI WA SHERIA NA MAMBO YA KATIBA TAREHE 03 APRILI, 2013 DODOMA

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania imekabidhi Taarifa mbili za Mapitio ya Mfumo wa Sheria unaosimamia Haki za Madai na Taarifa juu ya Sheria za Mila kwa Makabila yanayofuata mkondo wa mama kwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba Mh. Mathias Chikawe.

Makabidhiano ya taarifa hizo yamefanyika mkoani Dodoma baina ya Mwenyekiti wa Tume Mh. Jaji Aloysius Mujulizi na Waziri wa Sjeria na Mambo ya Katiba Mh. Mathias Chikawe na kuhudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo naibu Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba Mh. Angela Kairuki, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Fanuel Mbonde pamoja na Makamishna wa Tume ya Kurekebisha Sheria.

1. TAARIFA JUU YA MAPITIO YA SHERIA ZINAZOSIMAMIA HAKI ZA MADAI
Mapitio ya mfumo wa haki za madai ni moja kati ya juhudi mbalimbali za kuleta mabadiliko zinazochukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Programu ya Maboresho ya Mazingira ya Biashara Tanzania (BEST).

Katika kufanya utafiti wake Tume iliwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo Mahak**a na Mabaraza, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu,Taasisi zisizo za serikali, Jumuiya za Wafanyabiashara, Madalali, Mawakili na Taasisi na Idara za Serikali.

Katika kufanya utafiti, Tume ilijikita katika kufikia misingi ya utoaji haki k**a ilivyoainishwa na Ibara 107A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Misingi hii ni:-
• usawa – Yaani kutenda haki kwa wote bila kujali hali ya mtu kijamii au kiuchumi.
• uharaka – Yaani kutochelewesha haki bila sababu ya msingi.
• haki – Yaani kutoa fidia ipasayo kwa watu wanaoathirika kutokana na makosa ya watu wengine, na kwa mujibu wa sheria mahususi iliyotungwa na Bunge.
• usuluhishi – Yaani kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro; na
• utayari – Yaani kutenda haki bila kuweka msisitizo kwenye kanuni zinazoweza kukwamisha haki kutendeka.

Mradi huu unahusisha Mapitio ya Sheria tisa (9) na kanuni nane (8) zifuatazo:-
• Sheria ya Mamlaka ya Rufani, 1979 [Sura 141 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Usuluhishi, 1931 [Sura 15 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai, 1966 [Sura 33 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Ushahidi, 1967 [Sura 6 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Mashauri Dhidi ya Serikali, 1967 [Sura 16 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Mahak**a za Ardhi, 2002
• Sheria ya Ukomo wa Mashauri, 1971 [Sura 89 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Mahak**a za Mahakimu, 1984 [Sura 11 Mapitio ya 2002]
• Sheria ya Mabaraza ya Kata, 1985 [Sura 206 Mapitio ya 2002]Kanuni
• Muonekano wa Maafisa wa Serikali (Tangazo Na. 306 la Mwaka 1964)
• Mwenendo wa Mashauri ya Madai kwenye Rufaa zinazo tokea Mahak**a ya Mwanzo) Kanuni (Tangazo Na. 312 la Mwaka 1964)
• Tozo za Ada kwenye Mahak**a Kuu (Kitengo cha Biashara), 1999 (Tangazo Na. 275 lilofanyiwa marekebisho na Tangazo Na. 428 la mwaka 2005)
• Madalali wa Mahakamu Juu ya Uteuzi Wao, Malipo, na Udhibiti wa Nidhamu (Tangazo Na. 315 la Mwaka 1997);
• Tozo za Ada za Mahak**a (Tangazo Na. 308 la Mwaka 1964)
• Likizo za Mahak**a (Tangazo Na. 307 la Mwaka1964)
• Masijala za Mahak**a Kuu (Tangazo Na. 164 la Mwaka 1971)
• Lugha ya Mahak**a (Tangazo Na. 115 la Mwaka 1981)

Tume imefanya utafiti kwenye sheria zinazosimamia Haki za Madai kwa kubainisha mapungufu yaliyopo na kutoa mapendekezo ya namna bora ya kuboresha mapungufu husika. Tume inawasilisha taarifa ya Utafiti kwa Waziri wa Katiba na Mambo ya Sheria kwa hatua zaidi chini ya kifungu cha 15 cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria.

2. TAARIFA JUU YA SHERIA ZA MILA KWA MAKABILA YANAYOFUATA MKONDO WA UKOO WA MAMA
Tume ya Kurekebisha Sheria iliamua yenyewe kupitia sheria za mila kwa makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama. Itakumbukwa kuwa katika matamko ya serikali ya mwaka 20013, sheria za mila zilizoandikwa na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kuwa ni sheria za mila chini ya sheria za Tanzania zilikuwa ni sheria za mila kwa makabila yanayofuata ukoo wa Baba (Patrineal Societies). Hivyo Tume iliona umuhumu wa kuzitambua sheria za mila kwa makabiula yanayofuata ukoo wa mama na hatimaye kuziandika ili zijulikane kirahisi na kutumika kwenye maeneo ya makabila husika.

Tume ilifanya utafiti kwenye Wilaya za Kilombero, Kilosa, Ulanga Mvomero, Namtumbo, Tunduru, Ruangwa, Nachingwea, Masasi na Nanyumbu kwa nia ya kutambua sheria za mila zinzotumika kwenye wilaya hizo na hatimaye kuziandika. Wilaya hizi zilichaguliwa baada ya kubainika kuwa wakazi wake wanafuata mkondo wa ukoo wa mama. Tume imekamisha utafiti huu na inawasilisha taarifa ya utafiti kwa Waziri wa Katiba na Mambo ya Sheria kwa hatua zaidi chini ya kifungu cha 15 cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria

Address

Dar Es Salam
3580

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Law Reform Commission of Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Law Reform Commission of Tanzania:

Share