06/09/2026
“ENOUGH IS ENOUGH!” 💧🔥
«"Wiki mbili sasa bila maji huku kampuni za usambazaji maji zikiwa kimya. Cha kushangaza ni kuona biashara ya water buzzer ikiendelea kunoga. Hizi buzzer zinatoa wapi maji?"»
— Concerned Citizens
🚨 “HIZI WATER BUZZER ZINATOA WAPI MAJI?” WANANCHI WAIBUA MASWALI MAZITO KUHUSU MGOGORO WA MAJI 💧👀
Hasira za wananchi zinaendelea kuongezeka baada ya wiki mbili za ukosefu wa maji huku kampuni za usambazaji zikilaumiwa kwa ukimya wao. Kilichozua maswali zaidi ni kuonekana kwa malori ya kusambaza maji yakiendelea kufanya biashara k**a kawaida, jambo ambalo limewafanya baadhi ya wakazi kuhoji chanzo cha maji hayo wakati huduma rasmi zikidaiwa kusitishwa.
Mjadala sasa umehama kutoka kwenye ukosefu wa maji kwenda kwenye maswali ya nani anafaidika zaidi wakati wananchi wanahangaika kutafuta huduma hiyo muhimu. Je, ni bahati mbaya tu kwamba biashara ya water buzzer inanoga wakati mabomba yamekauka, au kuna kitu ambacho wananchi hawajaambiwa? 🤔💧