04/03/2022
*FIQH YA SAUMU.*
(Sehemu Ya 4)
*FAIDA ZA UCHAMUNGU.*
Nitaelezea kwa muhtasari tu fadhila anazopata mtu kwa kumcha Mwenyezi Mungu Alietukuka, fadhila hizo ni pamoja na mtu kuepushwa na mabalaa, kufundishwa elimu, kufutiwa madhambi na kusamehewa makosa, k**a ifuatavyo:
*Kutokana na kila dhiki.*
Mwenye kumkhofu Mola Mtukufu, akazishika amri zake, na akajitenga na makatazo yake, basi humjaalia njia ya kutokana na kila dhiki na balaa itakayompata. Anasema Allah Alietukuka:
๏ดฟูู
ูู ููุชูููู ุงููู ูุฌุนู ูู ู
ุฎุฑูุฌุงู๏ดพ.
โNa anayemuogopa Mwenyezi Mungu, (Mwenyezi Mungu) humtengenezea njia ya kuokoka (katika balaa). Na humpa riziki kwa namna asiotazamiaโ .
*Kuruzukiwa riziki kwa njia asioitegemea.*
Mwenye kumcha Mwenyezi Mungu basi atamtengezea njia na sababu za kuipatia riziki yake kwa njia na sababu ambazo yeye hakuzifikiria, na wala hakuzitegemea. Anasema Allah Alietukuka:
๏ดฟู ูุฑุฒูููู ู
ูู ุญูุซ ูุง ูุญุชุณุจ๏ดพ.
โ(Na anayemuogopa Mwenyezi Mungu)โฆ.. Na humpa riziki kwa namna asiotazamiaโ.
*Kufanyiwa mambo yake kuwa mepesi.*
Mwenye kumcha Mwenyezi Mungu Alietukuka basi atamrahishishia mambo yake, na kuona kila jambo litakalomsibu ni jepesi kwake. Anasema Allah Alietukuka:
๏ดฟููู
ูู ููุชูููู ุงูููููู ููุฌูุนูู ููููู ู
ููู ุฃูู
ูุฑููู ููุณูุฑุงู๏ดพ.
โNa anaye mcha Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu humfanyia mambo yake kuwa mepesiโ.
*Kupewa upambanuzi na kusamehewa madhambi.*
Ikiwa mtu atamcha Mwenyezi Mungu, basi Mola Alietukuka atampa utambuzi wa kutambua yale yaliyo ya batili miongoni mwa yale yaliyo ya kheri, na itakuwa ndio sababu ya kufutiwa madhambi yake. Anasema Allah Alietukuka:
๏ดฟุฅู ุชูุชูููููุงู ุงููู ููุฌูุนูู ูููููู
ููุฑูููุงูุงู ูู ูููููููุฑู ุนููููู
ู ุณููููุฆูุงุชูููู
ู ููููุบูููุฑู ููููู
ู ููุงููููู ุฐูู ุงูููููุถููู ุงูููุนูุธููู
ู๏ดพ.
โMkimcha Mwenyezi Mungu atakupeni tamyizi ya (upambanuzi) kupambanua baina ya haki na batili, na atakufutieni makosa yenu, na kukusameheni. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa sanaโ.
Kasema Abu Huraira Radhia Llahu Anhu aliulizwa Mtume Sallallahu Alayhi Wassallam:
ู
ููู ุฃูููุฑูู
ู ุงููููุงุณู.
โJee ni mtu gani mwenye heshima na taadhima,โ Akajibu akasema, โ
ุฃูุชูููุงููู
ู.
โYule anaemcha Mwenyezi Mungu zaidiโ.
ใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธใฐ๏ธ
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐จ๐ โ๐ ๐๐ฆ๐๐๐๐๐ค๐๐จ๐:
Faidika Na Mawaidha.
๐๐ถ๐๐ป๐ด๐ฒ ๐จ๐ณ๐ฎ๐ถ๐ฑ๐ถ๐ธ๐ฒ.
+255759801338
+255655559911
+96897822520