12/01/2023
Maisha ya Vyuoni huwa yanakupatia sio tu elimu ya darasani bali vile vile yanakukutanisha na elimu flani ya maisha. Ukiacha hatua k**a hiyo aliyochukua huyo kijana kwa mujibu wa Mwananchi, kuna wanachuo hufeli masomo yao kutokana na kuachwa/kuachika katika mahusiano ya kimapenzi. Mtu anampenda mwenzake kuliko anavyojipenda mwenyewe (anaenda beyond "Neighbourhood Principle"). Ukijipenda mwenyewe, hautakubali nafsi yako ipoteze malengo ya kile ulichokifuata Chuo kwa sababu ya mtu mwingine. Bahati mbaya unakuta mwingine anakuja kujifunzia mapenzi chuoni anakutana na mtu ambaye ameshagraduate kwenye masuala hayo akiwa secondari. Ukik**atwa kwenye mahusiano ya aina hiyo ndo ukiachwa unaona k**a dunia nzima aliyekuwepo ni huyo tu aliyekuacha. Na hapo sasa ndo inafikia mtu hataki kusoma, anatumia ada aliyopewa na wazazi wake kumuhudumia mtoto wa mtu, anawekw off campus k**a mpishi wa mwenzake anayeingia darasani, matokeo yake ukiachwa ni Discontinuation, kupata wendawazimu na hata kujinyonga. Maisha ya Chuoni ni lazima uyaendee kwa umakini ili kuweza kutimiza malengo yako, kuishi na wakubwa wenzio sio kazi ndogo. Ukitoka Chuoni, hutoki na degree tu, unatoka na experience nyingine za maisha. Katika jambo hili, TUPENDE KWA UMAKINI NA KIASI NA NAFSI YAKO NI BORA ZAIDI KULIKO MAPENZI.