28/05/2026
IJA, LEVO na GIZ WAENDELEA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA KUTOA ELIMU YA SHERIA LUSHOTO
Katika kuendelea kuimarisha uelewa wa jamii kuhusu maana, vyanzo na athari za ukatili wa kijinsia pamoja na masuala mbalimbali ya sheria, Chuo cha Uongozi wa Mahak**a Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Asasi ya Kiraia ya Kisheria ya Legal Vision Organization (LEVO), kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Ujerumani (GIZ), wametoa elimu ya kisheria na msaada wa sheria kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.
Zoezi hilo, ambalo litachukua siku sita, tayari limefanyika katika makanisa ya EAGT, TAG na Katoliki, Soko la Lukozi, Shule ya Sekondari Lukozi, Shule ya Msingi Lukozi, Kiwanja na Mng'alo pamoja na kwa makundi ya akina mama na waendesha bodaboda wa maeneo ya Mnazi na Mng’alo.
Elimu hiyo ilianza kutolewa Mei 24, 2026 ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kuhamasisha jamii kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na kujenga mazingira salama yenye usawa, haki na heshima kwa wote.
Kupitia kampeni hiyo, wananchi wameendelea kuelimishwa kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia, umuhimu wa kulinda haki na utu wa kila mwanajamii pamoja na wajibu wa jamii kushiriki kikamilifu katika kutokomeza vitendo hivyo.
Zoezi hilo linaendeshwa na wahadhiri na maafisa sheria kutoka IJA, wasaidizi wa kisheria kutoka LEVO pamoja na maafisa kutoka GIZ.
Kutoka IJA yupo Mhadhiri Msaidizi Bw. Roggers Cletus, Maafisa Sheria Bi. Jackline Kulwa na Bw. George Banoba. Kutoka LEVO wapo Bw. Miraji Abdalah Malinda, Bi. Doris Maiko Kiungulia, Bi. Diana Godfrey pamoja na Bw. Gadson Wilfred Honkonyo.
Aidha, kutoka GIZ wapo Mshauri wa Sheria Bi. Neema Ndemno na Mtaalamu wa Mawasiliano, Uhamasishaji na Kampeni Bi. Agnes Mwafifi.
Hii ni awamu nyingine ya kampeni ya utoaji wa elimu na msaada wa sheria inayotekelezwa na GIZ, IJA na LEVO kwa jamii ya Lushoto, ambapo awamu ya awali ilifanyika mwezi Septemba mwaka 2024.
Aidha, GIZ imekuwa mstari wa mbele katika kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia ambapo katika kipindi cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ili waleta pamoja Mahakimu Wakazi, Mawakili wa Serikali, Polisi dawati la jinsia, viongozi wa dini, wa kimila.