25/10/2025
Tarehe 17 Octoba 2025, Wadau wa Kampeni ya na Kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo waliadhimisha Siku ya Mwanamke anayeishi Kijijini ambayo huadhimishwa Kila mwaka tarehe 15 Octoba. Maadhimisho haya yalifanyika Kijiji Cha Kaole, kata ya Dunda.
Maadhimisho haya yaliambatana na mjadala juu ya umuhimu wa kuimarisha na kusimamia haki za Ardhi za Mwanamke hasa anayeishi Kijijini, uhitaji wa kushirikisha wanawake kwenye harakati na maamuzi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Maadhimisho haya yaliambatana na uzinduzi rasmi wa Ilani ya Haki za Ardhi za Mwanamke, inayotoa wito na madai ya wanawake wa Tanzania juu ya umiliki wa Ardhi, nafasi katika maamuzi na utawala wa Ardhi, elimu ya sheria na msaada wa kisheria, upatikanaji wa rasilimali na uwezeshwaji, pamoja na uwajibikaji. Nyenzo hii itatumika na wanawake katika kufanya uchechemuzi wa haki zao.
Huduma ya Msaada wa kisheria pia ilitolewa na ikiwa na sehemu ya kuhakikisha ulinzi na usimamizi wa haki unatendeka.
Maadhimisho haya yalihudhuriwa na wajumbe wa Jukwaa la wanawake wa vijijini kutoka nchi za SADC linaliratibiwa na ambayo walitoa uzoefu kutoka nchi zao. Vilevile wawakilishi kutoka Kiteto, kilosa, ifakara, kilombero, Mlimba, Loliondo na maeneo ya karibu na Bagamoyo.