16/05/2026
Wanandoa wengi wenye utaifa tofauti wanapofunga ndoa hujikuta wakijiuliza mwongozo wa kisheria utakaotumika iwapo watataka kutalikiana, kugawa mali walizochuma pamoja, na kuamua hatma ya ulezi wa watoto wao, hasa pale mali na watoto wanapokuwa katika mataifa tofauti.
Kwa wanandoa ambao mmoja ni Mtanzania na ndoa ilisajiliwa nchini, mahak**a za Tanzania zina mamlaka ya kusikiliza shauri la talaka, ambapo wito wa mahak**a hutolewa na kufikishwa kwa mwenza wa kigeni kupitia balozi wa Tanzania katika nchi anakokaa au kupitia dalali wa mahak**a walioteuliwa na Mahak**a Kuu.
Mali zilizopo Tanzania hugawanywa kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa ya Tanzania kwa kuzingatia mchango wa kila mmoja, huku ushahidi wa mwenza aliye nje ya nchi ukiwasilishwa kwa njia ya affidavit na Ikiwa ni ushahidi wa mdomo, mahak**a inaweza kutumia video conference. Mali zilizopo nje ya Tanzania hugawanywa kwa mujibu wa sheria za nchi husika, kwani mahak**a za Tanzania hazina mamlaka ya kugawa mali nje ya mipaka yake.
Kwa upande wa watoto, iwapo wapo Tanzania, mahak**a hutumia Sheria ya Ndoa kwa kuzingatia kanuni ya ustawi wa mtoto, na ulezi unaweza kutolewa kwa mzazi yeyote kulingana na maslahi ya watoto; lakini iwapo wapo nje ya Tanzania, sheria za nchi wanapoishi ndizo zitatumika kuamua hatma ya ulezi, ingawa jukumu na haki za wazazi hubaki za kudumu.
Vilevile, k**a ndoa ilisajiliwa katika nchi ya kigeni, taratibu za talaka, mgawanyo wa mali na malezi ya watoto hutolewa kwa kutumia sheria za nchi husika, lakini iwapo mali zingine na watoto wapo nchini Tanzania, basi Sheria ya Ndoa ya Tanzania itatumika kugawa mali na kutoa ulezi wa watoto kwa wazazi hao.
Baada ya hukumu ya talaka kutolewa Tanzania, hutumwa kwa balozi wa Tanzania ili kuwasilishwa kwa mahak**a ya nchi ya mwenza wa kigeni kwa uthibitisho na utambuzi wa uhalali wa talaka hiyo, na vivyo hivyo hukumu ya talaka iliyotolewa nje hutumwa Tanzania kupitia balozi na Wizara ya Mambo ya Nje ili mahak**a za Tanzania ziiidhinishe na kuitambua rasmi.
NUKUU
Sheria inalinda haki zako
Kutojua sheria si sababu ya kushindwa kutumia haki zako. Kwa maelezo zaidi, wasiliana nami kupitia 0654819753 kwa WhatsApp au simu.
Imeandaliwa na Hussein